Monday, November 06, 2006

Ditopile atuhumiwa kuua!


Mkuu wa mkoa wa Tabora Kapteni Ukiwaona Ditopile Mzuzuri, ametiwa mbaroni na Polisi kwa tuhuma za mauaji ya raia kwa kutumia bastola yake, jijini Dar es salaam, Tanzania.
Habari kutoka eneo la tukio zilizothibitishwa na kamishina wa Polisi Kanda maalum ya Dar es salaam, Alfred Tibaigana zinaeleza kuwa Ditopile anatuhumiwa kumuua papo hapo Dereva wa daladala Hassan Mbonde mkazi wa Kawe Mzimuni jijini Dar kwa kumpiga risasi kichwani.
Dito anatuhumiwa kumuua dereva huyo juzi saa 2:30 usiku katika njia panda ya barabara ya Kawe na Bagamoyo, wilaya ya Kinondoni baada ya kuchukizwa na hatua ya gari lake kugongwa kwa nyuma na gari lililokuwa likiendeshwa na marehemu.
Gari lililokuwa likiendeshwa na marehemu ni Isuzu Journey linalofanya biashara ya daladala kati ya Ubungo na Tegeta, huku gari ya Dito ikiwa ni aina ya Toyota Prado iliyokuwa ikiendeshwa na Nassoro Mohamed (42) ambalo lilivunjwa taa ya nyuma katika ajali hiyo.

0 Comments:

Post a Comment

<< Home