Wednesday, December 20, 2006

Mawaziri Lowassa na Sumari!


Waziri Mkuu Lowassa na Naibu Waziri wa Kazi Jeremia Sumari wakiwa na wake zao wakisubiri kumpokea Rais Kikwete katika ukumbi wa Ubungo Plaza kulikofanyika sherehe ya harusi ya watoto zao, Pamela na Sioi!

Rais Kikwete Harusini!


Rais wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete akiingia katika ukumbi wa Ubungo Plaza katika sherehe ya harusi ya watoto wa Mawaziri katika serikali yake yake.
Watoto hao wa Waziri Mkuu Edward Lowassa (Pamela)na Naibu Waziri wa Kazi Jeremia Sumari (Sioi)walifunga ndoa Jumamosi iliyopita Desemba 16, 2006! Mungu aijaalie ndoa yao idumu milele!

Tuesday, December 12, 2006

Siri ya umri wa Beyonce yafichuka!


Ikiwa zimepita siku chache tangu kukumbwa na tuhuma za 'kumwagwa' na mpenzi wake Jay Z, hivi karibuni mwanadada Beyonce Knowles ameibukiwa na tuhuma zingine za utata juu ya umri wake halisi.
Tuhuma hizo za aina yake zimedai kuwa, mwanamuziki huyo amedanganya mashabiki wake juu ya umri wake halisi, ambapo kwa kipindi kirefu amekuwa akijitambulisha kuwa na umri wa miaka 25 kutokana na kuzaliwa Setpemba 4 mwaka 1981, jambo linalodaiwa kuwa si kweli.
Ikadaiwa zaidi kuwa, umri halisi wa binti huyo ni miaka 32 kutokana na kile kilichodaiwa kwamba ni kuzaliwa mnamo mwaka 1974, huku tarehe na mwezi wa vikibaki kama alivyojitangaza.

Banza awajibika jukwaani!



Mwanamuziki Banza Stone akiwajibika jukwaani sambamba na mwanamuziki mwingine wa bendi ya African Stars au Twanga Chipolopolo, Angelo walipozindua albamu yao ya Hujafa Hujasifiwa kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee Jumamosi Desemba 8, 2006

Banza Stone katika Uzinduzi!



Mwanamuziki nguli wa bendi ya African Stars Twanga Chipolopolo Ramadhani Masanja au Banza Stone akiingia ndani ya Ukumbi wa Diamond Jubilee katika onesho la Uzinduzi wa albamu ya bendi hiyo inayokwenda kwa jina la Hujafa Hujasifiwa!

Monday, December 04, 2006

Haya kula Keki Amina!


Mheshimiwa Mbunge wa Viti maalum (CCM) Amina Chifupa Mpakanjia akilishwa keki na mumewe Mohamed Mpakanjia kwenye sherehe ya kumbukumbu ya miaka sita ya ndoa yao na miaka mitano ya mtoto wao Rahman Mpakanjia! Sherehe hiyo ilifanyika nyumbani kwao Sinza jijini Dar.

Friday, November 24, 2006

Kuna Ukweli katika Hili?!

Kuna uvumi huku Bongo unadai kuwa uhusiano wa Jay Z na Beyonce eti hauko sawa kwa sasa, ambapo Beyonce 'analiwa' na Usher Raymonds huku Jay Z naye 'anamla' Rihanna, eti wachunguzi wa mambo hebu nisaidieni katika hilo!

Beyonce Na Usher - video powered by Metacafe

Kanisa la St Peter Osterbay


Kanisa hili lipo Osterbay, Dar jirani kabisa na Makao Makuu ya Usalama wa Taifa, historia ya kipekee kwa kanisa hili ni ibada zake kuhudhuriwa mno na viongozi wa Serikali ya Tanzania na hata maofisa wa balozi mbalimbali zilizopo Bongo!
Hapa ndo hayati Mwl Julius Nyerere alikuwa na sehemu yake maalum, si unajua tena huyu alikuwa neva miss katika Ibada!

Viwanja vya Disko Siku hizi Kibao!


Siku hizi 'viwanja' vya disko vimekuwa vingi sana Bongo tofauti na zamani, Kuna JJ Club, Bar One, Garden Bistro, Arabella na vingine kibao, kila wikiendi ni kuruka kwanja kwa kwenda mbele... Zamani ilikuwa Billz sijui na Mambo Club, mtanisaidia zaidi wadau!
Hiyo hapo pichani ni kiwanja cha Garden Bistro kiko mitaa ya Masaki!

Thursday, November 23, 2006

Ray C Anakuja na Albamu ya Pili!


Mtoto wa kike Rehema Chalamila au Ray C, aliwahi kuvuma sana redioni akiwa mtangazaji wa East Africa Radio (Radio One Channel three)na baadaye Clouds FM amenitumia Email ya kunihabarisha kuwa albamu yake imeshaiva, hivyo anatarajia kuitoa siku si nyingi!

Hebu nawe icheki barua pepe yake hapa chini...
Mambo vipi? Albamu yangu ina nyimbo kumi na moja nakutajia baadhi ya majina...

Tabasamu lako (REGGAE)
Wawili (ZOUK)
Siangalii nyuma feat Dgritty mdogo wake Loon
Nilikutamani feat TID
Mapenzi ya kweli
Kama wanipenda feat Pfunk
Sogea Sogea
Sogea sogea remix
Sugadaddy
Kwa ajili yako feat Nako 2 Nako
Niacheni

Album itatoka mwezi ujao mwanzoni, nimerekodi studio tofauti ambazo ni Metro Studio, Mandugu Digital na Bongo Records!

Juma Nature Ajitoa TMK Wanaume Family!


Mwanamuziki mahiri wa Bongo Flava, Juma Kassim au Sir Nature ambaye hivi karibuni aliwania moja ya tuzo za MTV Base maeripotiwa kujitoa katika kundi lake Wanaume TMK baada ya kutokea kutoelewana kati yao!
Meneja wa kundi hilo, Said Fella alithibitisha kujitoa kwa msanii huyo akiwa na wasanii wengine wa kundi hilo, D Chief, Dolo na Luten Kalama, kwa kile alichokieleza kuwa ni tabia ya ubinafsi ya wasanii hao!
Wasanii wengine waliobaki, wametanabaisha kuwa, kuondoka kwa wasanii hao hakuwafanyi kutoendelea na 'kukamua' hivyo wametuhakikishia kuwa yale 'mapanga shaa' yataendelea!
Hata hivyo kuna fununu kuwa wasanii hao waliojitoa katika kundi hilo, wanatarajia kuungana na Inspekta Haroun au Babu na kuibuka na kundi lao jipya linalotarajia kuanza mambo yake hivi karubini, isitoshe wimbo mpya wa Nature na Inspekta uitwao Hakuna Kuremba unatarajia kutoka hivi karibuni!

Tuesday, November 21, 2006

Ditopile Alia na Rais Kikwete, Shein!



Aliyekuwa mkuu wa Mkoa wa Tabora Ndugu Ukiwaona Ditopile Mzuzuri wamelaani kitendo cha vingozi mbalimbali wa Serikali wakiwemo Rais Jakaya Kikwete na Makamu wake Dk Ally Mohamed Shein kwenda kutoa rambirambi kwa familia ya aliyekuwa dereva wa daladala Hassan Mbonde anayedaiwa kuuawa na bw Ditopile!

Mawakili wa Ditopile wakiongea kwa niaba yake walisema kuwa kitendo cha viongozi hao kwenda kuhani kwa familia ya dereva huyo kwa ving'ora na promo za nguvu kunatoa sura ya kumtia hatiani Dito kabla ya mahakama kuthibitisha hilo, hivyo kuitaka Mahakama kuzuia rambirambi hizo mara moja!

Hata hivyo Mahakama hiyo ya Kisutu imelitosa ombi hilo, kwa kile kilichoelezwa kuwa mahakama haifanyii kazi mambo yanayotokea mitaani, Dito amerudishwa tena rumande hadi kesi itakapotajwa tena!

na Irene Mark
MWANASHERIA maarufu wa kimataifa, Nimrod Mkono, amechukua jukumu la kuwa kiongozi wa jopo la mawakili wa utetezi wa aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Ukiwaona Ditopile - Mzuzuri, anayekabiliwa na mashitaka ya mauaji.
Mkono, ambaye ni Mbunge wa Musoma Vijijini (CCM), sasa anaungana na mawakili wengine wanne. Mawakili hao ni Dk. Ringo Tenga, Cuthbert Tenga, Rosan Mbwambo, na Samuel Mapande.
Jana Mkono alisimama mahakamani Kisutu, na kuanza kumtetea mteja wake, akianza na hoja ya kupinga viongozi mbalimbali wa serikali, kwenda kuhani nyumbani kwa marehemu, Hassan Mbonde, ambaye alikuwa dereva wa daladala.
Alidai mbele ya Hakimu Mfawidhi, Michael Luguru, kwamba kitendo cha viongozi wa serikali kwenda nyumbani kwa mfiwa si kumtendea haki mteja wao, kwa kuwa anakuwa amekwisha kuhukumiwa kwamba ameua.
“Viongozi wa nchi wanaokwenda kumwona mfiwa na kutoa rambirambi wanatupa wasiwasi kama haki itatendeka.
“Hivi Jaji Mkuu akiamua kwenda kutoa pole, itakuwaje? Spika akienda, hata wewe Mheshimiwa hakimu, itakuwaje?”
“Wanakwenda na vinolinoli (ving’ora) na kutoa pole na fedha, vyombo vya habari vinaandika, hii inaweza kusababisha haki kutotendeka kwa mtuhumiwa, mahakama iwapige marufuku hawa,” alidai Mkono.
Alivishukuru vyombo vya habari kwa kuandika ziara za viongozi wa serikali nyumbani kwa mfiwa, kwa kuwa bila hivyo jamii isingefahamu kwamba familia ya marehemu inatembelewa na viongozi hao.
Mkono alisema kitendo kilichofanywa na viongozi wa serikali, ni ukiukwaji wa Ibara ya 13 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ibara hiyo inasema watu wote ni sawa mbele ya sheria, na ni marufuku mtu kubaguliwa kwa namna yoyote ile.
Alisema ziara hizo zimefanywa nyumbani kwa wazazi na familia ya wafiwa pekee, na kwamba ingekuwa haki kama viongozi hao pia wangemtembelea mteja wake mahabusu ambako anaendelea kushikiliwa.
Baadhi ya viongozi waliokwenda kuhani ni Katibu Mkuu Kiongozi, Philemon Luhanjo, ambaye alimwakilisha Rais Jakaya Kikwete na kutoa ubani wa sh 500,000.
Pia Makamu wa Rais, Dk. Ali Mohamed Shein; Meya wa Kinondoni, Salum Londa; na wengine wengi, wamekwisha kwenda kuhani.
“Kila siku matukio ya kuuawa yanatokea, lakini hatuwaoni kwenda…basi kama wanataka kwenda wachukue likizo au waende kwa siri, huu ni ukiukwaji wa Katiba,” alidai Mkono.
Akijibu hoja za wakili huyo, Mrakibu Mwandamizi wa Polisi (SSP) Charles Kenyella, alidai kwamba mahakama haifanyi kazi kwa kusikiliza maneno ya watu au matendo ya viongozi wa serikali.
Alimtaka wakili huyo kutokuwa na wasiwasi juu ya utendaji wa haki.
Baada ya hoja na majibu ya pande zote, Hakimu Luguru, alisema kwa kuwa mahakama hiyo haina uwezo kisheria wa kusikiliza kesi za mauaji, haiwezi kutoa agizo lolote.
Alisema malalamiko ya wakili huyo wa utetezi yanawekwa katika maandishi, yakaamuliwe na Mahakama Kuu.
Kesi hiyo iliahirishwa hadi Desemba 4, mwaka huu, itakapotajwa tena. Upelelezi haujakamilika.
Ilidaiwa kwamba Novemba 14, mwaka huu, kwenye makutano ya Barabara ya Bagamoyo na Kawe, Dar es Salaam, Ditopile-Mzuzuri, alimuua Hassan Mbonde, kwa kumpiga risasi.
Kama ilivyokuwa wiki mbili zilizopita mahakamani hapo, jana Ditopile-Mzuzuri, alikuwa mnyonge, na muda wote alionekana kujiinamia.
Mkono wake wa kulia ambao inadaiwa kwamba aliumizwa kwenye eneo la tukio, haukuwa na bandeji; hali iliyofanya kovu kubwa lionekane.
Jana alivaa shati la kitenge lenye rangi ya kijani kikavu, suruali nyeusi na balaghashia nyeupe.
Kuwapo kwa Mkono katika kesi hiyo, kunaongeza mvuto, kwani ni nadra mno kwa wakili huyo kusimama katika kesi za kawaida.
Kesi ambayo aliweza kuonekana ni ile ya kumtetea mfanyabiashara, Valambia.
Mkono anatambuliwa na kuheshimika kimataifa, kama mmoja wa mawakili maarufu na wenye mafanikio makubwa katika fani ya sheria.
Hivi karibuni alipokea tuzo ya kimataifa nchini Uingereza.
Wakati huo huo, Mkono alitoa hoja hizo mahakamani, Mnajimu Sheikh Yahya Hussein, juzi aliitembelea familia ya marehemu Mbonde na kuahidi kumtibu kiharusi, mama wa marehemu.
“Wameonyesha kufarijika sana kwa michango mbalimbali iliyotolewa na viongozi wa kiserikali, kisiasa, kidini na watu binafsi…kama mtumishi wa Kurani
nimewaomba na wameniruhusu niwapeleke Hijja watu wawili kutoka kwenye familia yao akiwamo baba mzazi wa marehemu.
“Maandalizi kwa ajili ya ahadi hiyo nimeanza kuyatekeleza leo (jana),” alisema.

http://www.freemedia.co.tz/daima/2006/11/21/habari1.php

Sunday, November 19, 2006

Ajali!


Mzee huyu ambaye jina lake halikutambulika jana mida ya saa kumi hivi alipata ajali ya gari wakati akivuka barabara ya Lumumba maeneo ya Mnazi Mmoja, Dar! Aliteguka kiuno na kupasuka kichwa, dereva alijikata bila kutoa msaada wowote, lakini namba zilidakwa na wasamalia wema... Mzee akakimbizwa Muhimbili kwa matibabu!
Hapa baadhi ya watu wakimshuhudia mzee huyo baada ya kugongwa!