Thursday, November 23, 2006

Juma Nature Ajitoa TMK Wanaume Family!


Mwanamuziki mahiri wa Bongo Flava, Juma Kassim au Sir Nature ambaye hivi karibuni aliwania moja ya tuzo za MTV Base maeripotiwa kujitoa katika kundi lake Wanaume TMK baada ya kutokea kutoelewana kati yao!
Meneja wa kundi hilo, Said Fella alithibitisha kujitoa kwa msanii huyo akiwa na wasanii wengine wa kundi hilo, D Chief, Dolo na Luten Kalama, kwa kile alichokieleza kuwa ni tabia ya ubinafsi ya wasanii hao!
Wasanii wengine waliobaki, wametanabaisha kuwa, kuondoka kwa wasanii hao hakuwafanyi kutoendelea na 'kukamua' hivyo wametuhakikishia kuwa yale 'mapanga shaa' yataendelea!
Hata hivyo kuna fununu kuwa wasanii hao waliojitoa katika kundi hilo, wanatarajia kuungana na Inspekta Haroun au Babu na kuibuka na kundi lao jipya linalotarajia kuanza mambo yake hivi karubini, isitoshe wimbo mpya wa Nature na Inspekta uitwao Hakuna Kuremba unatarajia kutoka hivi karibuni!

0 Comments:

Post a Comment

<< Home