Thursday, November 09, 2006

Mama Hambiliki Afariki Dunia!


Mugizaji wa kundi sanaa la Kaole la jijini Dar Mama Hambiliki amefariki kutokana na kuugua maradhi ya moyo yaliyomsumbua kwa miezi miwili kabla ya kuzidiwa Alhamisi iliyopita na kukimbizwa Hospitali ya Mwananyala kwa matibabu zaidi ambapo aliaga dunia juzi usiku
Kwa mujibu wa mtoto wa marehemu Shuruti Saidi (49), siku za hivi karibuni hali ya marehemu mama yao ilianza kubadilika na mara kwa mara alikuwa akilalamika kuhusu ugonjwa wa moyo uliofanya afya yake kuzorota siku hadi siku. .
”Miezi miwili hivi iliyopita mama alianza kuugua maradhi ya moyo na daktari alituambia moyo wake umekuwa mkubwa, hivyo alianza kutumia dawa kabla ya Alhamisi iliyopita kuzidiwa na tulimpeleka wananyamala kwa matibabu zaidi lakini kwa bahati mbaya amefariki,” alisema Shuruti.
Alisema kifo cha mama yao kimeacha pengo kubwa kwa familia hiyo kwa vile alikuwa mhimili kutokana na juhudi zake za kutetea, kulinda na kutoa miongozo thabiti kwa wote.
Msanii huyo aliwahi kuvuma katika sanaa ya uigizaji kabla ya Uhuru na kutamba katika vipindi mbalimbali vya michezo vilivyokuwa vikirushwa hewani na Sauti ya Dar es Salaam (TBC) ambayo baadaye iliitwa Redio Tanzania Dar es Salaam na baada ya kuibuka kwa vituo mbalimbali vya televisheni nchini alijiunga na kundi maarufu la Kaole.
Mungu aiweke mahali pema, roho ya marehemu...amina

0 Comments:

Post a Comment

<< Home