Thursday, November 16, 2006

Filamu ya Kimataifa ya Kanumba kuzinduliwa Dar!


Filamu ya Kimataifa ya Dar 2 Lagos iliyotungwa na kuchezwa na muigizaji mahiri wa filamu nchini Steven Kanumba maarufu kama Kanumba inataraji kuzinduliwa kwa mara ya kwanza nchini Tanzania mwishoni mwa mwezi huu.
Filamu hiyo inayofungua ukurasa mpya katika anga za filamu nchini, hasa kutokana na kushirikisha wasanii wa mbili tofauti nchi pamoja na kurekodi katika mbili tofauti bila kusahau ndani ya ndege ikiwa angani na kuigizwa kwa umahiri mkubwa na waigizaji hao nyota.
Akiongea na mwandishi wa habari hizi, mtunzi huyo alisema kwamba filamu hiyo iliyotumia lugha za Kiingereza na Kiswahili ilianza kurekodiwa jijini Dar es salaam kabla ya kwenda kumaliziwa vipande vingine nchini Nigeria kulingana na muongozo wa filamu hiyo.
Akasema kwamba, filamu hiyo imewashirikisha waigizaji wawili toka nchini Tanzania, ambao ni Emmanuel Myamba pamoja naye huku waigizaji toka Nigeria wakiwa Mercy Johnson na Bimbo Akintoe pamoja na washiriki wengine.
Uzinduzi huo utakaofanyika Novemba 30 mwaka huu, unatarajiwa kufanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam sambamba na burudani zingine toka kwa waigizaji mahiri nchini kama Kiwewe, Mtanga, Masele, Matumaini na wengineo pamoja na bendi za African Stars 'Twanga Pepeta' na 'Twanga Chipolopolo'.
Aidha, baadhi ya wasanii wa maigizo toka nchini Nigeria watakakuwemo katika uzinduzi huo ambapo wanaotarajiwa kuwasili nchini katikati ya mwezi huu ni Emanuel Francis, Nkiru Silvanus pamoja na walioshiriki katika 'muvi' hiyo.
Filamu hiyo imeandaliwa na kampuni ya Game 1st Quality ya jijini Dar ambayo ni mmoja wa wadhamini wa uzinduzi huo wakishirikiana na Dotnata Decoration nayo ya jijini Dar.

0 Comments:

Post a Comment

<< Home