Thursday, November 16, 2006

Wapiga kura wametamka:
Kura zimepigwa kutafuta saa ya mkutano wa kwanza kabisa wa wanablogu na wapenzi wa blogu wa Tanzania. Mkutano utafanyika saa nane mchana saa za Tanzania, Novemba 18, 2006.

Wapiga kura waliochagua saa nane mchana wameshinda. Hakuna masanduku ya kura yaliyoibwa wala kura zilizoharibika. Wala hakuna pingamizi lolote.

Maandalizi ya mkutano yanaendelea katika ukurasa wa wiki ambao utaupata kwa kubonyeza hapa. Tafadhali shiriki kwenye maandalizi. Ukipata tatizo la jinsi ya kuweka maoni yako kwenye ukurasa wa maandalizi ya mkutano, bonyeza hapa usome maelezo mafupi.

Kura 22 zimepigwa kuchagua saa nane mchana kwa saa za Tanzania
Kura 19 zimepigwa kuchagua saa sita mchana kwa saa za Tanzania
·
Hivyo: Mkutano wa wanablogu na wapenzi wa blogu wa Tanzania ni tarehe 18 Novemba, 2006, saa nane mchana saa za Tanzania.

Kama unataka kujua saa nane za mchana Tanzania ni saa ngapi hapo ulipo (kama upo nje ya TanzaMkutano huu utafanyika kupitia teknolojia ya Internet Relay Chat, hivyo utakuwa ni mkutano wa mtandaoni. Bonyeza HAPA uende kwenye tovuti ya mkutano.

Maelezo:

Maelezo haya ni muhimu sana maana usipoyafuata hutaweza kushiriki.
1. Nenda kwenye tovuti ya IRC@Work (http://www.ircatwork.com/)
2. Ukifika hapo utakuta kisanduku kina sehemu tatu.
3. Sehemu ya kwanza inasema Nickname. Andika jina lako kwenye kisanduku hicho.
4. Sehemu ya pili inaitwa Server. Usiandike chochote au kubadili chochote hapo
5. Sehemu ya tatu inaitwa Channel, hapo utaandika: #blogubongo
6. Baada ya kufanya hivyo, bonyeza pale panaposema Login
7. Utakuwa umeingia ndani ya ukumbi wa mkutano.
8. Ukishaingia, upande wa juu kulia utaona majina ya watu wengine walioko ukumbini.

Ukitazama chini kabisa utaona ufito mwembamba ambao ndio utautumia kuandika mchango wako kwenye mkutano. Ukishaandika unabonyeza Enter kwenye kompyuta yako ili mchango wako usomwe.



ILANI

Watu wengi tunajiuliza blogu ni kitu gani? Tunatembelea blogu, tunazisoma, tunashawishika kutaka kuanzisha zetu, ila bado tunakuwa tunajiuliza, “blogu ni nini?” Soma makala alizoandika Mfalme wa Blogu Ndesanjo Macha kujaribu kutoa jibu la swali hili. Makala hizi ziko katika sehemu tatu. Bonyeza hapa.

Pia kuna makala fupi katika Wikipedia ya Kiswahili inayojibu swali: blogu ni nini? Bonyeza hapa uisome.

0 Comments:

Post a Comment

<< Home