Wednesday, December 20, 2006
Rais Kikwete Harusini!
Rais wa Tanzania Jakaya Mrisho Kikwete akiingia katika ukumbi wa Ubungo Plaza katika sherehe ya harusi ya watoto wa Mawaziri katika serikali yake yake.
Watoto hao wa Waziri Mkuu Edward Lowassa (Pamela)na Naibu Waziri wa Kazi Jeremia Sumari (Sioi)walifunga ndoa Jumamosi iliyopita Desemba 16, 2006! Mungu aijaalie ndoa yao idumu milele!
Tuesday, December 12, 2006
Siri ya umri wa Beyonce yafichuka!
Ikiwa zimepita siku chache tangu kukumbwa na tuhuma za 'kumwagwa' na mpenzi wake Jay Z, hivi karibuni mwanadada Beyonce Knowles ameibukiwa na tuhuma zingine za utata juu ya umri wake halisi.
Tuhuma hizo za aina yake zimedai kuwa, mwanamuziki huyo amedanganya mashabiki wake juu ya umri wake halisi, ambapo kwa kipindi kirefu amekuwa akijitambulisha kuwa na umri wa miaka 25 kutokana na kuzaliwa Setpemba 4 mwaka 1981, jambo linalodaiwa kuwa si kweli.
Ikadaiwa zaidi kuwa, umri halisi wa binti huyo ni miaka 32 kutokana na kile kilichodaiwa kwamba ni kuzaliwa mnamo mwaka 1974, huku tarehe na mwezi wa vikibaki kama alivyojitangaza.